6/13/18

FAHAMU MBEGU ZA NYONYO/MBARIKA

Utangulizi

Mbarika ama nyonyo (castor seeds) ni mbegu za daikotiledoni ambazo zipo katika kundi la mbegu zitoazo mafuta, kundi moja na mbono kaburi (jatropha). Mmea wa nyonyo kitaalamu hujulikana kama 'ricinus communis'. Katika jamii nyingi za Kiafrika, mbegu za mmea huu zimekuwa zikitumika kutengeneza mafuta kwa ajili ya kulainisha ngozi za wanyama na kuwashia taa.
Mimea ya nyonyo ni sumu, kwa hivyo hailiwi na wanyama na husitawi maeneo mengi, hata yale yaliyo na ukame.

Picha: Mmea wa nyonyo/mbarika





Picha: Mbegu za nyonyo/mbarika, kabla hazijakomaa.

MATUMIZI

Mmea wenyewe hutumika kama uzio hai (live fence)
Katika baadhi ya jamii, majani ya mmea huu hutumika kukanda (massage) na kutibu maumivu yatokanayo na kuteguka.
Mbegu za nyonyo husagwa, huchemshwa na kuenguliwa mafuta. Mafuta ya nyonyo huweza kusafishwa katikaa mitambo ya kisasa na kutumika kuendeshea mitambo kama dizeli ya mimea (biodiesel). Pia hutumika kutengenezea mafuta ya kulanisha mitambo. Kumbuka kuwa mafuta ya kulainisha mitambo aina ya Castrol hutengenezwa kutokana na mmea huu.

13 comments:

John Mwaipopo said...

Mzee nilikuwa sijatembelea blogu siku nyingi imekolea kinoma. Itafunika sana hii.

Alex Mwalyoyo said...

Sawa mkuu PF, tuendelee kuiboresha!

Unknown said...

Elimu nzuri, je hulimwa wapi na upatikanaji wa Mbegu upoje

JOHANES DEUSDEDIT said...

Iko vizuri hii blog.Mimi binafsi napenda sana masuala ya kulima ila sijawa na uchaguzi sahihi maana kila nikisikia zao fulani lina tija nakuwa na hamasa kweli kutaka kujua zaidi juu ya zao hilo hata kusoma katika mitandao mbali mbali.Niko na chaguzi nyingi sana za kukipenda kilimo na kufanya kilimo Cheney tija baada ya masomo yangu ya chuo kikuu nutakavyo hitimu hapo mwaka kesho.Naomba ushauri wenu kityuu gani haswa cha kulima nikipata faida maan mimi napenda kulima magapi,strawberry,mihogo,pilipili n.k....

JOHANES DEUSDEDIT said...

Pia naomba elimu zaidi kuhusu mbarika kilimo chake,faida zake,na soko likoje kwa hapa Tanzania na nje ya Tanzania

Unknown said...

Naomba km kuna faida zaidi za mmea huu Wa mnyonyo

Unknown said...

Unawashauri nini kuhusu mmea huu?????

Unknown said...

Ni nzury hii elimu na inahitajika kuifanyia kazii

Unknown said...

Nakusudia project zifanyike kwa hii elimu hasa ya kutengeneza mafuta ni muhim sana

Unknown said...

Naomba kujua nazipata je nazihitaj sana

Unknown said...

Nahitaji kulima hili zao la nyonyo kwa wingi kabisa naomba nipate ufafanuzi wa soko lakee

Anonymous said...

Daaaaaaaah me nahitaji dawa yakukuza uume 0783639377

Anonymous said...

Me nataka dawa za syphilis