6/13/18

Jiunge na Harakati za Siku ya Blogu Duniani

Siku ya Blogu ni ipi?
UtanguliziNi tukio ambalo linawakutanisha waandishi na wamiliki wa blogu duniani kujadili kuhusu mada moja ambayo huwa imechaguliwa na kisha kuweka mada hiyo katika blogu zao anuwai. Siku hii ni tarehe 15 Oktoba ya kila mwaka na imekuwa ikiadhimishwa tangu mwaka 2007. Matukio ya siku hii huratibiwa na mtandao uitwao ‘Blog Action Day’ (http://blogactionday.org) .

Mada za Siku ya Blogu
Kwa miaka ya nyuma, mada zilizowahi kujadiliwa ni umasikini (ufukara), maji na mabadiliko ya tabianchi. Mwaka jana 2010 mada iliyokuwa imechaguliwa ilihusu maji, kwa hiyo wanablogu duniani kote tulishiriki katika majadiliano kwa njia ya mtandao kuhusu suala la maji, kwa upana wake. Binafsi, nimeandika mada anuwai kuhusu maji na mazingi (kwa kuwa ndiyo taaluma yangu ilikoegemea). Mwaka huu, siku ya blogu duniani imesogezwa mbele kwa siku moja ili kushabihiana na siku ya chakula duniani (tarehe 16 Oktoba), kwa hiyo mada kuu ya mwaka huu inahusu CHAKULA! Kwa maana hiyo basi, wanablogu mbalimbali duniani wataandika mada mbali mbali kuhusu chakula, iwe ni upatikanaji wake, uhifadhi, uandaaji, matumizi, uharibifu, maadili katika usindikaji, ulafi, uhaba na namna tunavyowezesha upatikanaji wa chakula kwa jamii zote duniani na kadhalika.
Unakaribishwa kushiriki katika majadiliano haya, pia unaweza kujisajili katika mtanda wa Blog Action Day katika anuani niliyoiweka hapo juu!
Ahsante sana.

No comments: