Blogu hii ipo kwa ajili ya kuelimisha jamii kuhusu masuala mbali mbali ndani ya jamii hii pana, hasa masuala ya mazingira, nishati na maendeleo endelevu. Ingawa taarifa zilizo katika tovuti hii zinatolewa bure kwa ajili ya kuongeza uelewa katika jamii,si vibaya kama utataka kunakili ama kuzitumia, ila ni vyema na ni ustaarabu kama utataja kuwa umezitoa hapa. Asante
6/13/18
BARAFU YA MLIMA KILIMANJARO
Mlima Kilimanjaro ni mrefu kuliko mlima wowote ule hapa barani Afrika ukiwa na urefu wa meta 5895 juu ya usawa wa bahari. Juu ya mlima huu pamefunikwa na barafu. Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na tafiti mbali mbali zikieleza namna barafu hiyo inavyoyeyuka kwa kasi kutokana na ongezeko la joto duniani (nimewahi kuliongelea kwa kina suala hili katika makala zilizopita). Kwa sasa kumekuwa na juhudi mbali za makusudi za kupunguza athari hizi, huenda kukawa kuna mafanikio siku za baadaye kama tutashirikiana kutunza mazingira kuzunguka mlima huu.
Kibo na Mawenzi
Kilele cha Mawenzi
Kilele cha Kibo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment