5/22/06

UKO HURU KUNENA!

Karibu katika blogu hii. Hapa tutakuwa tukijadili mada mbali mbali pamoja na kutoa maoni katika mada husika.
Zingatia kuwa Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (toleo la 1998) sura ya kwanza sehemu ta tatu, ukurasa wa 23 ibara ya (18) (1) kinachohusu uhuru wa mtu kutoa mawazo yake , kinatamka bayana kuwa 'bila kwenda kinyume cha sheria za nchi, kila mtu ana haki na uhuru wa kutoa mawazo/fikra zake, na kutafuta, kupokea na kusambaza taarifa au fikra kwa kutumia njia yeyote ile, bila kujali mipaka ya nchi na ana haki ya ya kutoingiliwa katika mawasiliano au mpashano huu wa habari'. (2) 'Kila raia ana haki ya kupashwa habari muda wote kuhusu matukio mbali mbali katika nchi na dunia kwa ujumla wake, ambayo ni muhimu kwa watu na maisha yao na muhimu kwa jamii nzima pia.'
Hivyo basi, ni kwa kutumia uhuru huu ambapo blogu hii inafanya kazi , na ndugu msomaji/mchangiaji upo huru kuchangia mawazo yako kwa mada tutakazokuwa tunaziweka hapa.

1 comment:

Ndesanjo Macha said...

Safi sana ulivyotupa kifungu cha katiba kuhusu uhuru wa kutoa mawazo.