5/22/07

MWAKA MMOJA WA KUJADILI WATIMIA!

TOVUTI YATIMIZA MWAKA
Leo tarehe 22/05/2007 tovuti hii inatimiza mwaka mmoja tangu izinduliwe rasmi mwaka jana 2006. Tarehe kama hii mwaka jana ndipo makala ya kwanza ilibandikwa mahali hapa. Nakumbuka jinsi ilivyokuwa vigumu kuamua cha kuandika, lakini hatimaye mambo yakaenda vyema na mpaka leo naendelea kusimama.
Tangu izinduliwe rasmi mwaka jana, tuvuti hii imefanyiwa madiliko ya mwonekano mara tatu na bado itaendelea kuboreshwa kwa kuongeza mambo mapya ambayo kwa sasa yanaandaliwa.
Kimsingi mawazo ya kuanzisha blogu hii yalitokana na ushawishi mkubwa wa Mzee wa "Baragumu", ambaye ni swahiba wangu wa siku nyingi sana, tangu tukiwa tunasoma shule moja ya sekondari mkoani Iringa. Huyu ndiye aliyenishawishi kwa kiasi kikubwa kuanzisha tovuti hii na baadaye akafuatiwa na mwanablogu nguli, Mzee wa "Jikomboe". Pamoja na hawa pia kuna kundi kubwa sana la wanablogu wenzangu ambao naweza kuujaza ukurasa huu kama nitaamua kuwataja mmoja baada ya mwingine ambao wamekuwa wakitoa michango yao mbali mbali ya mawazo katika kuiboresha tovuti hii, hawa nao nawapa shukrani za pekee.
Nayathamini sana mawazo yenu na naomba tuendelee kushirikiana ili tuweze kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kuboresha mazingira yetu.
Naahidi kuendelea kuweka makala za kuzua mijadala ya kuboresha maisha yetu mahali hapa, na naomba tuendelee 'kujadili' kama kawaida yetu.

No comments: