10/3/12

Tanesco na ombi la maboresho kutoka kwa walaji (Consumers)

Utangulizi Ofisi ya mahusiano ya Tanesco imetoa tangazo (pichani) ikiomba maoni ya wateja kuhusu maboresho ambayo wanataka kuyafanya, ili kuongeza ufanisi wa shirika hilo. Shirika hili ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi, hivyo ufanisi wake ni nguzo muhimu sana kwa ukuaji wa uchumi wetu kwa ujumla. Ushauri Mimi ni mdau wa nishati katika taifa hili na pia ni mteja wa Tanesco. Kuna mada fulani (iko hapa) niliiweka katika blog hii siku za nyuma kuhusu matatizo yanayoisibu Tanesco na namna ya kupunguza kama si kuondoa kabisa matatizo hayo. Tanesco ina vitengo vitatu muhimu, ambavyo ni uzalishaji umeme (Generation), usafirishaji umeme (Transmission) na ugavi umeme (Distribution). Shida kubwa sana ya Tanesco ipo katika generation na distribution. Ningeomba watendaji wakuu (menejimenti na bodi)za shirika hili wazingatie ushauri niliowapa hata robo tu,watafikia hilo lengo wanalolitafuta. Ushauri wangu umewahi kutolewa na wataalamu wengine wengi tu akiwamo Januari Makamba. Lakini pia wasome (na ikiwezekana kutekeleza) mapendekezo ya ripoti iliyoandaliwa na Benki ya Dunia kuhusu upotevu wa umeme. Ni hayo tu. Tuendelee na mjadala