6/13/07

NAFASI ZA UONGOZI KATIKA JUMUIYA YA WANABLOGU WA TANZANIA

OMBA NAFASI ZA UONGOZI
Ndugu msomaji wa blogu hii, kuna nafasi mbali mbali za uongozi zimetangazwa katika Jumuiya ya Wanablogu wa Watanzania. Unaruhusiwa kugombea nafasi yoyote, na si lazime uwe na blogu ili kupata nafasi hizo. Nafasi hizo zinazonadiwa ni za Mwenyekiti, Mhazini, Katibu na nyinginezo.

MAMBO YA KUZINGATIA
Tuma picha yako ukiambatanisha na wasifu wako, pamoja na sababu zinazokutuma kugombea na nafasi unayogombea. Ueleze ni kitu gani unataka kuifanyia Jumuiya katika kuikuza. Tuma maelezo yako kwa 'mijasayi@yahoo.com'.
Kwa maelezo zaidi tafadhali tembelea blogu ya Jumuiya 'http://blogutanzania.blogspot.com'

No comments: